5/30/2005

TAZAMA VIDEO YA MAHOJIANO YANGU AFRIKA KUSINI

Nimewasili Babiloni. Safari nzima nilikuwa najiuliza, "Hivi nitablogu nini na nini nitaacha?" Kwanza hata pa kuanzia sijiu. Nimeamua kuwa nitakuwa nablogu kila siku mambo kadhaa yaliyotokana na mkutano wa Commons-sense; mambo niliyojifunza, watu niliokutana nao, miradi mbalimbali inayotumia zana mpya za mawasiliano Afrika, niliyoona katika jiji la Egoli/Jozi (majina ya jiji la Johannersburg), mapana na marefu ya dhana hii ya "creative commons" (bado natafuta tafsiri yake sahihi ya Kiswahili), n.k.

Ndio nimeamka nataka kunywa chai. Ningependa kwa sasa utazame video hii ya mahojiano niliyofanya na New Media Lab ya chuo kikuu cha Rhodes. Bonyeza hapa uitazame.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com