5/05/2005

WAKATOLIKI NA MATAMBIKO, BLAIR NA AFRIKA!

Rafiki yangu kanitumia ujumbe alioandikiwa na rafiki yake. Ujumbe mfupi ila kataja mambo mengi. Siwataji majina yao ila nauweka ujumbe wenyewe hapa. Huo hapo chini:
Kwanza nimesikitishwa sana na mambo ya matambiko na uchawi uliokuwa unafanyika kwenye uchaguzi wa Papa. Hivi ule moshi mweusi na mweupe ni nini kama sio uchawi au tambiko. Hivi mwafrika ndio akifanya mbwembwe na matambiko kama vile ndio unakuwa uchawi ila mzungu yeye akifanya ni "utaratibu tu uliozoeleka kwa muda mrefu." Hivi na hii Tume ya Blair inayotaka kumaliza matatizo ya nchi za Afrika umeiona? Ina watu wanaitwa maprofesa mle ndani. Mimi nadhani wale ni maprofesa wa ujinga maana akili zao ni ndogo kuliko binadamu yeyote niliyewahi kumuona. Hawajawahi kusoma historia na hoja zao ni hafifu sana. Eti wao hawajui matatizo yao na wala hawajui namna ya kuyatatua mpaka wasaidiwe na Blair. Kuhusu uchaguzi wa Tanzania mimi sitaki kabisa kusumbua kichwa changu kuhusu nani atakuwa Rais. Huwa ni rahisi sana kumtambua mwenye uwezo kati ya wanyonge ila ni ngumu sana kumtambua mpuuzi sana kati ya wapuuzi wengi. Hivi ni nani angehisi kuwa mwaka 1995 nchi hii ingemhitaji mtu mwenye sera za kipuuzi kama hizi za Mkapa na utandawazi wake? Hivi mtu kama hauwezi kutumia rasilimali zako dawa ni kuzitoa kwa mtu mwingine ili azitumie badala ya wewe kujenga uwezo wa kuzitumia hata kama ni miaka 500? Nadhani ukibahatika kujua ni nani mpuuzi kuliko wagombea hao wote utamjua Rais anayefuata maana nadhani hizi nchi za kiafrika ili sifa zao zitimie ni kuwa na kiongozi mpuuzi.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com