6/06/2005

G8 SUMMIT KUJADILI AFRIKA

Kama ambavyo baadhi wanavyojua, Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair, anasema kuwa moja ya kazi zake kubwa ni kuhakikisha kuwa bara la Afrika linanyanyuka toka katika dimbwi la umasikini, migogoro, ukimwi, n.k. Kwahiyo moja ya mada kuu katika kikao cha viongozi wa nchi tajiri 8 duniani unaofanyika huko Uingereza mwezi ujao ni Afrika. Soma hapa. Blair ni mwenyekiti wa Kamisheni/Tume ya Afrika ambayo mmoja wa makamishna wake ni rais wa Tanzania, Benjamin Mkapa. Tume hii imetoa ripoti yake inayopatikana hapa. Ukienda hapa unaweza kuona na kusikiliza yaliyosemwa wakati wa uzinduzi wa ripoti yenyewe.
Ukiacha Mkapa, kamishna mwingine toka Tanzania ni mama Anna Tibaijuka. Makamishna wengine hawa hapa.
Hapo awali viongozi wa G8 waliunda NEPAD kule Kanada. Haya ndio madhumuni ya NEPAD. Tunajua tunakokwenda?




0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com