6/24/2005

Tutakutana na George Monbiot

Waandishi tunaokwenda nchini Uingereza katika mpango wa shirika la Panos uitwao G8 Media Fellowship, tumefahamishwa kuwa asubuhi ya tarehe 5 mwezi ujao tutakutana na mwandishi na mtangazaji nimpendaye wa siasa za mrengo wa kushoto, George Monbiot. Monbiot huwa anaandika makala za kila wiki katika gazeti la the Guardian la Uingereza. Licha ya kuandika magazetini, Monbiot pia ni mtunzi wa vitabu kama vile The Age of Consent: A Manifesto for a New World Order, Captive State: The Corporate Takeover of Britain, Poisoned Arrows, na No Man’s Land (alichokiandika kutokana na ukachero alioufanya Kenya na Tanzania). Monbiot, ambaye ameishi na kufanya kazi Indonesia, Brazil, na Afrika ya Mashariki, ni mwalimu wa muda katika chuo kikuu cha Oxford Brookes. Tembelea tovuti yake kwa habari zaidi juu yake na makala na insha mbalimbali za upembuzi yakinifu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com