7/04/2005

Blogu mbalimbali za G8

Unaweza pia kufuatilia yanayotokea hapa kupigia blogu hizi maalum kwa ajili ya wezi nane, G8:
Gazeti la the Guardian, blogu ya Paul Mason wa BBC Newsni8t, blogu ya Open Democracy , blogu ya gazeti la Red Pepper , IndyMedia nchini Uskoti na Technorati.
Nasikia kuwa katika viongozi waliokaribishwa kuwa watazamaji kwenye mkutano wa viongozi waliojichagua wenyewe kuwa ndio wapitisha sera kuu za uchumi wa dunia hii ni rais wa Tanzania, Benjamin Mkapa. Nitamtafuta nipige naye picha niweke ukutani ili nije kuwaonyesha vitukuu wangu wakati nikiwapa historia ya jinsi bara letu lilivyochukuliwa na makampuni toka nje.
Wakati wa maandamano makubwa ya Make Poverty History nilifanya nilihojiana na Waafrika waliotoka Afrika kuja Uskoti kuandamana. Kuna makala niliyoandika ikiuliza kijiji alichozaliwa Tony Blair huko Afrika.

1 Maoni Yako:

At 7/05/2005 02:57:00 PM, Anonymous Anonymous said...

KWANINI WAAFRIKA TUNAFUATILIA SANA HUU MKUTANO?

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com