7/05/2005

Kuondoa umasikini ni kuondoa ubepari

Kuna harakati za wabunge hawa toka nchi mbalimbali duniani za kutaka Benki ya Wezi (benki ya dunia) na shirika ambalo bango moja kwenye maandamano ya jumamosi lilisema kuwa kirefu chake ni International Mother F**** (IMF) yaendeshwe kidemokrasia. Hivi sasa kura za wanachama wa vyombo hivi vya kibaguzi zinategemea uwezo wa kiuchumi wa nchi. Kwahiyo utaoana kuwa Marekani ikitaka kupitisha au kupinga jambo lolote kwenye vyombo hivi watafanikiwa bila kipingamizi chochote. Na jamaa hawa ndio wanasema kuwa wanataka kuifundisha dunia demokrasia.
George Monbiot alisema jambo moja zuri sana jana. Alisema kuwa akina Bono na Geldoff wanashindwa kujua jambo moja muhimu sana: hakuna uwezekano wa kubadili vyombo hivi vya njururu. Vyombo hivi vimeundwa ili kuendeleza matakwa ya nchi tajiri ambazo zinategemea sana umasikini wa nchi za Kusini. Umasikini wa nchi zetu ndio njia pekee ya kuwafanya wao kuwa matajiri. Usitegemee, kwa mfano, Waswisi wataipa Ghana msaada wa kujenga viwanda vya kutengeneza chocolate. Waswisi wanataka kununua cocoa toka Ghana kwa ajili ya viwanda vyao, Ghana ikiwa na uwezo wa kutengeneza chocholate wenye viwanda Uswisi unataka wale polisi?
Monbiot anasema kuwa hakuna njia yoyote ya kuondoa umasikini duniani bila kuhoji, kukabiliana, na kuuondoa mfumo wa ubepari unaowapa viongozi wachache na makampuni ya maswahiba wao au makampuni yenye hisa zao uwezo wa kuamua jambo lolote kwa niaba ya dunia nzima.
Tazama sura halisi ya mfumo huu wa ubepari: makampuni ya Makidonadi na Walt Disney yanatumia fedha za matangazo kwa mwaka mzima ambazo ni zaidi ya bajeti ya elimu na afya ya nchi 18 duniani.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com