7/02/2005

Mtanzania aliyekuja Edinburgh

Asubuhi leo niliondoka na waandishi Machrine na Maura kwenda katika kanisa la Uskochi pembeni na jumbe la makumbusho hapa Edinburgh. Kulikuwa na mkutano kuhusu wakulima na mabadiliko ya hali ya hewa. Katika mkutano huo Davinder Sharma wa Forum for Biotechnology and Food Security (India) alisema kuwa wakati watu zaidi ya 20,000 wanakufa kwa njaa nchini India, nchi hiyo inazalisha kwa mwaka chakula cha akiba ambacho ukikiweka kwenya magunia ya kuyapanga moja juu ya jingine, kutakuwa na uwezekano wa magunia hayo kufika kwenye nyota. Mkulima toka Burkina Faso alitumkubusha kuwa maana ya neno Burki Na Faso: "Nchi ya watu waaminifu." Lakini furaha ya kuhudhuria mkutano huu niliipata pale jamaa mmoja aliponiuliza, "Wewe si Ndesanjo?" Huyu alikuwa ni Joseph Mzinga, Mtanzania anayefanya kazi nchini Zambia. Mzinga yuko hapa Edinburgh akiwakilisha sauti ya wakulima wa Afrika katika harakati za kupinga tamaa ya kundi la nchi nane.

Kuna tatizo limetoa nashindwa kupata kidude cha rangi na wakati mwingine kidude cha kuweka viungo. Najaribu kutafuta chanzo.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com