8/08/2005

Je Mwanamke ni haki kuendesha swala ya kiislamu?

Ametishiwa kuuawa. Wako watu wanataka kabisa kuondoa uhai wake kutokana na mawazo na fikra zake. Badala ya kupambana naye hoja bin hoja na fikra juu ya fikra baadhi wanaona kuwa dawa ni kumuua. Ulevi wa dini ni ulevi mbaya sana. Unaweza kuondoa kabisa uwezo wa kufikiri. Kama mtu una mawazo tofauti na yangu kwanini nikuue?
Sijui kama umewahi kumsikia Profesa Amina Wadud ambaye anatia hasira sana baadhi ya waislamu kutokana na mawazo yake kuhusu uislamu. Huyu ndiye mwanamama ambaye mwaka 1994 aliongoza swala msikitini nchini Afrika Kusini na mapema mwaka huu aliongoza sala ya kiislamu ndani ya kanisa la kikristo baada ya misikiti mitatu kumkatalia. BBC wana habari kuhusu tukio hilo. Profesa Wadud katika swala hiyo, kama ilivyo kawaida yake, alikuwa akimuita mungu wa kiislamu, Allah, kwa kutumia vijina vya kiume na kike toka lugha ya kiingereza, yaani "He" na "She" maana anaamini kuwa ni kosa kumpa mungu jinsia moja tu yaani ya kiume kama inavyofanywa kwenye uislamu (nami naongeza: hata kwenye kitu kiitwacho ukristo). Na hili ndio tangazo la swala ya kiislamu aliyoendesha kanisani.
Waislamu walimjia juu sana alipohutubia Canada mwanzoni mwa mwaka huu. Hapa anasahihisha baadhi ya yaliyoripotiwa katika habari kuhusu hutba yake hiyo ya Canada.
Profesa Wadud ambaye alizaliwa katika familia ya Kimethodisti na baadaye aliingia katika imani ya Kibudha kwa muda mfupi kabla ya kuingia dini ya waarabu ya kiislamu ni mwalimu wa masuala ya uislamu katika idara ya Falsafa na Dini katika chuo kikuu cha Virgnia Commonwealth. Mwaka 1992 aliandika kitabu hiki hapa. Profesa
Kuna mahojiano yake hapa ambapo kati ya mambo anayosema ni kuwa ni kosa kubwa ya "sharia" ambayo imetokana na mfumo dume kuongelea masuala ya wanawake wakati ambapo wanawake hawakuhusishwa katika kuunda vipengele hivyo vya sharia vinavyowahusu. Pia unaweza kusoma mawazo yake zaidi na kutazama na video yake hapa. Kuna hutba yake nyingine hapa kuhusu Maandiko, Jinsia, na Mageuzi katika Uislamu.
Soma zaidi juu ya tafsiri tofauti ndani ya uislamu juu ya wanawake kuongoza swala kama maimamu.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com