10/21/2005

Pop!Tech: Bart Depram anaongea

Bart Depram anajihusisha na mradi wa kutengeneza zana za kusaidia watu kutumia mtandao wa kompyuta kama sehemu ya kujenga mahusiano. Anasema wafanyabiashara wanataka kufanya webu kuwa ni kama soko moja kubwa. Yeye na wenzake wanataka kufanya webu iwe ni sehemu ya maingiliano, mahusiano, n.k.
Naandika anayosema bila kusahihisha:
- tazama webu yao ya www.flock.com
(nimetazama pembeni nikapitwa. Ameitaja tovuti hii: http://secondlife.com/ ila sijui kwanini ameitaja maana sentensi za awali zikuzisikia. Sasa anaonyesha teknolojia wanayotengeneza ambayo inakusanya habari mbalimbali toka kwenye tovuti mbalimbali. Kwa teknolojia hii huna haja ya kwenda kwenye tovuti hizo)
**************
Sasa wazungumzaji wote wameketi jukwaani wanaulizwa maswali. Kiti moto.
Negroponte akijibu swali kuhusu wakazi wa vijijini na watoto wa shule watakavyotunza kompyuta hizo: anasema wamefanya majaribio huko Cambodia na kukuta kuwa watoto wakiona matumizi ya kompyuta hizo watazitunza.
Negroponte anaulizwa je mtu akitokea mtu akitaka kununua kwa dola 300?
Anajibu kuwa kompyuta hizo hazitauzwa kwa kila mtu. Ni kwa ajili ya kusaidia watoto katika nchi zinazoendelea.
(Ninaacha kusikiliza ili nikaongee na jamaa fulani. Wakimaliza tunakwenda kula mlo wa jioni).

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com