10/20/2005

Pop!Tech: Marcia na utafiti chini ya habari

Marcia McNutt anaongea hivi sasa kuhusu utafiti chini ya bahari. Anasema utafiti wa sayari za mbali una faida kadhaa ambazo ni changamoto kwa watu wanaotafiti chini ya bahari. Kwa mfano, anasema mawasiliano chini ya bahari ni magumu zaidi ya mawasiliano kati ya dunia na watafiti walioko sayari za mbali. Pia anasema utafiti angani unafaidika kwa nishati ya jua wakati ule wa chini ya bahari unatumia zaidi betri. Hivi sasa anatuonyesha chombo kiitwacho Autonomous Underwater Vehicle. Chombo hiki anasema ndio macho, mkono, masikio na kila kitu kwa wanasayansi wanaotafiti yaliyoko chini ya ardhi. Chombo hiki kinajiendesha chenyewe, kina kamera zenye uwezo wa kuona kila kitu, kina mikono, n.k.

(Mawazo Yangu: Sijui kwanini wanafanya utafiti wa mamilioni chini ya bahari...hivi hawajui chini ya bahari kuna nini? Chini ya bahari kuna chunusi na majini mengine kama jini mahaba...)!

Anaongelea viumbe vipya ambavyo vimegunduliwa kutokana na utafiti wao. Anasema kuna aina ya funza ambaye hana mdomo, tumbo, wala mfumo wa kusaga chakula. Anazungumzia viumbe vingine ila tuache utani hapa anaanza kuniacha nje. Majina tu ya viumbe hao na mimea chini ya ardhi...acha tu. Sijui kwanini nilikuwa nakwenda kujificha nyuma ya chooni na Richard Shilangale na Ramadhani Isa wakati wa kipindi cha baiolojia pale shule ya Mawenzi. Naamini ningejua kidogo anayozungumzia.

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com