10/21/2005

Pop!Tech: Rebecca wa Global Voices anaongea

Hivi sasa anaongea Rebecca Mackinnon wa mradi wa Sauti za Dunia (Global Voices) anaongea hivi sasa. Mjadala wake unaitwa How the Internet is Changing China. Blogu yake hii hapa.

Anaongelea kijiji kimoja huko China kilichojenga tovuti hii: www.pusalu.com mwaka 1999. Tovuti hii ilitokana na madai kuwa kijiji hicho kimekuwa kikitembelea na viumbe toka sayari nyingine. Kijiji hicho kimepata umaarufu kiasi ambacho utalii kijijini hapo umekuwa ni sehemu kubwa ya kuwapatia fedha. Anasema serikali ya China inatumia mamilioni ya dola hivi sasa ili kusaidia vijiji nchini humo kuwa na mitandao ya Intaneti.

Akizungumzia jinsi ambavyo mtandao wa kompyuta unabadili mambo huko China, Rebecca anatoa mifano kadhaa. Mfano wa kwanza unahusu mwanablogu maarufu China ambaye umaarufu wake unatokana na urahisi wa watu binafsi kutoa habari mtandaoni. Mwanablogu huyu ni binti mmoja mrembo ambaye anaandika masuala mbalimbali kuhusu maisha yake. Mamilioni ya wasomaji hutembelea blogu yake.

Mfano mwingine unahusu mwalimu mmoja ambaye alikuwa anaishi maisha ya kawaida hadi pale aliporekodi wimbo na kuuweka mtandaoni. Wimbo unaitwa: Mice Love Rice. Wimbo wake umesikilizwa na watu zaidi ya milioni 100 mtandaoni. Tayari amepata mkataba wa kurekodi na anazunguka kila mahali akitumbuiza.

Anaendelea...

0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com