11/01/2005

Je Blogu Zinaidharau Afrika?

Ethan Zuckerman kazua mjadala mkali. Siku zinavyokwenda unapamba moto. Anasema kuwa blogu, kama vilivyo vyombo vikubwa vya habari havipendi kuandika mambo yanayohusu Afrika. Anasema blogu zinapenda kuandika zaidi mambo kuhusu teknolojia. Ametoa mifano miwili toka blogu ya Boing Boing. Ili upate uhondo wenyewe bonyeza hapa. Ukishasoma aliyoandika, soma na maoni ya wasomaji wake (hapo ndio kuna uhondo hasa).

1 Maoni Yako:

At 11/02/2005 05:40:00 AM, Blogger mwandani said...

Mjadala huo safi sana. Kitu kimoja kimenigusa - ni vipi kila mmoja wetu, kwa uwezo wake, ataweza kuondoa matatizo ya Afrika, siyo tu kwa kulalamika kwamba vyombo vya habari haviandiki masuluhisho ya matatizo yetu...
naamini tunao ufunguo, ama funguo nyingi tu... Ni jinsi gani tunaweza kuzitumia ndio swala...

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com