11/16/2005

Kenya: Sakata la Kura ya Maoni

Kundi moja linalojiita vuguvugu la Njano lilikwenda mahakamani likitaka zoezi la kupiga kura ya maoni ya "ndiyo" au "hapana" kuhusu katiba mpya nchini Kenya lisimamishwe. Kundi hili lilidai kuwa bunge lilipounda sheria ya kutengeneza katiba mpya lilijichukulia mamlaka ambayo yako mikononi mwa wananchi. Pia likadai kuwa tume ya uchaguzi ya Kenya haina haki kisheria kusimamia zoezi hilo maana tume hii imepewa wajibu wa kusimamia uchaguzi wa wabunge na rais na sio kura ya maoni kuhusu katiba. Wanasheria wa kundi hili walidai kuwa kesi hii pengine ni kesi ya pili kwa ukubwa nchini Kenya ukiachilia mbali ile ya shujaa Dedan Kimathi. Jana Mahakama Kuu nchini Kenya imeamua kuwa zoezi hilo litaendelea. Bonyeza hapa usome habari hiyo.
Wakati huo huo jamaa wa Kenya National Commission of Human Rights ambao wanafuatilia kwa karibu kampeni za kura hii ya maoni, wana "orodha ya aibu" katika tovuti yao. Orodha hii inaonyesha matumizi mabovu ya mali ya umma na kauli za uchochezi toka kwa waongo na wezi wanaojiita wanasiasa nchini humo. Bonyeza hapa utazame orodha hiyo.




0 Maoni Yako:

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com