1/07/2006

Somo, Ngoma, na Tambiko la Kwanzaa





















Nikifundisha watoto (unajua tena samaki mkunje angali mbichi) maana ya Kwanzaa na umuhimu wake kwa watu wenye asili ya Afrika. Katika picha nyingine hiyo: huyo ni Barry akifungua somo la Kwanzaa kwa ngoma baada ya kutoa tambiko. Barry ni Mmarekani Mweusi ambaye amejifunza kupiga ngoma aina ya Djembe katika nchi ya Guinea, Afrika Magharibi. Mikono yake migumu kama tairi la nyuma la trekta aina ya Kubota (hivi Makubota yaliishiaga wapi?). Juu ya Kwanzaa soma niliyoandika hapo chini na pia bonyeza hapa.
Bonyeza juu ya picha zenyewe uzione kwa karibu zaidi.

1 Maoni Yako:

At 1/08/2006 01:02:00 PM, Blogger boniphace said...

Ndesanjo mimi nashukuru huu utaratibu wa kutuwekea vipicha maana vinatuwezesha kuwa karibu na tukio na kufahamiana zaidi. Kazi njema hao ni muhimu kwani zama zao zipo mbele kuliko zetu

 

Post a Comment

<< Home

FREE hit counter and Internet traffic statistics from freestats.com